99

Mungu mtawala mkuu
1 Mwenyezi-Mungu anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameketi juu ya viumbe vyenye mabawa, nayo dunia inatikisika!
2 Mwenyezi-Mungu ni mkuu katika Siyoni; ametukuka juu ya mataifa yote.
3 Wote na walisifu jina lake kuu la kutisha. Mtakatifu ndiye yeye!
4 Ee mfalme mkuu, mpenda uadilifu! Umethibitisha haki katika Israeli; umeleta uadilifu na haki.
5 Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu; angukeni kifudifudi mbele zake. Mtakatifu ndiye yeye!
6 Mose na Aroni walikuwa makuhani wake; Samueli alikuwa miongoni mwa waliomlilia. Walimlilia Mwenyezi-Mungu naye akawasikiliza.
7 Alisema nao katika mnara wa wingu; waliyazingatia matakwa yake na amri alizowapa.
8 Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza; kwao ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliwaadhibu kwa makosa yao.
9 Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu; abuduni katika mlima wake mtakatifu! Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Generic placeholder image