93
Mungu mfalme 1 Mwenyezi-Mungu anatawala; amejivika fahari kuu! Mwenyezi-Mungu amevaa fahari na nguvu! Ameuimarisha ulimwengu, nao hautatikisika kamwe. 2 Kiti chako cha enzi ni imara tangu kale; wewe umekuwapo kabla ya nyakati zote. 3 Vilindi vimetoa sauti, ee Mwenyezi-Mungu; naam, vimepaza sauti yake, vilindi vyapaza tena mvumo wake. 4 Mwenyezi-Mungu ana enzi kuu juu mbinguni, ana nguvu kuliko mlio wa bahari, ana nguvu kuliko mawimbi ya maji. 5 Ee Mwenyezi-Mungu, maagizo yako ni thabiti; nyumba yako ni takatifu milele na milele.