64

Sala ya kuomba ulinzi wa Mungu
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1 Usikie, ee Mungu, lalamiko langu; yalinde maisha yangu na vitisho vya maadui.
2 Unikinge na njama za waovu, na ghasia za watu wabaya.
3 Wananoa ndimi zao kama upanga, wanafyatua maneno ya ukatili kama mishale.
4 Toka mafichoni wamshambulia mtu mnyofu, wanamshambulia ghafla bila kuogopa.
5 Wanashirikiana katika nia yao mbaya; wanapatana mahali pa kuficha mitego yao. Wanafikiri: “Hakuna atakayeweza kuiona.”
6 Hufanya njama zao na kusema: “Sasa tumekamilisha mpango! Nani atagundua hila zetu?” Mipango ya siri imefichika moyoni mwa mtu!
7 Lakini Mungu atawapiga mishale, na kuwajeruhi ghafla.
8 Atawaangamiza kwa sababu ya maneno yao; kila atakayewaona atatikisa kichwa.
9 Hapo watu wote wataogopa; watatangaza aliyotenda Mungu, na kufikiri juu ya matendo yake.
10 Waadilifu watafurahi kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu, na kukimbilia usalama kwake; watu wote wanyofu wataona fahari.

Generic placeholder image