ALHAMISI JUMA 25 LA MWAKA WA 1
MASOMO
SOMO 1: Hag.1:1-8
Katika mwaka wa pili wa Dario mfalme, mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana
lilimjia Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda na Yoshua, mwana wa Yeosadaki, kuhani
mkuu, kwa kinywa chake Hagai nabii, kusema, Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, watu hawa
husema, hu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujengwa nyumba ya Bwana. Ndipo neno la
Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika
nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika? Basi sasa. Bwana wa
majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini
hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na
yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka. Bwana wa majeshi asema
hivi, Zitafakarini njia zenu. Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia,
nami nitatukuzwa, asema Bwana.
WIMBO WA KATIKATI: Zab.149:1-6,9 (K)4
1. Aleluya,
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Sifa zake katika kusanyiko la watauwa!
Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,
Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao!
(K) Bwana awaridhia watu wake.
2. Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie!
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba wenye upole kwa wokovu. (K)
3. Watauwa na waushangilie utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Na upanga mkali kuwili mikononi mwao. (K)
4. Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa:
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. (K)
SHANGILIO: Zab.25:4,5
Aleluya, aleluya!
Unijulishe ee Bwana unifundishe mapito yako
Aleluya!
INJILI: Lk.9:7-9
Herode mfalme alisikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine
walisema ya kwamba Yohane amefufuka katika wafu, na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na
wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka. Lakini Herode akasema, Yohane
nilimkata kichwa; basi ni nani huyu ambaye ninasikia mambo haya juu yake? Akataka kumwona.
--------------
--------------
MAOMBI
Ndugu, Mungu anapenda kila jumuiya ya waamini iwe
na mahali rasmi pa kukutana naye. Kwa vile mahali hapo
ni mfano wa makao yake ya milele huko mbinguni, tusali
tukisema:-
Kiitikio: Pokea ombi letu.
1. Ubariki juhudi za Askofu wetu F., ili kila jumuiya
ya waamini ihamasike kuwa na nyumba bora ya
ibada, upate kukutana nao humo kwa utulivu. Ee Bwana.
2. Viongozi wa serikali wajaliwe moyo wa ushirikiano
na Wachungaji wetu katika kuleta hali bora ya maisha
ya watu wako kimwili na kiroho. Ee Bwana.
3. Wabatizwa wote tuongezewe ari ya kulitii neno lako
linalohubiriwa kwetu na Wachungaji uliowatuma
kwetu badala yako. Ee Bwana.
4. Katika mkanganyo na ubatili wa mambo, utujalie
kujikabidhi kwako ambako kuna maana ya mwisho
na ya uhakika juu ya mambo yote. Ee Bwana.
5. Ndugu zetu marehemu wapate ufufuo na uzima wa
milele huko mbinguni. Ee Bwana.
Ee Mungu unayetaka tuushuhudie ukweli, uyapokee
maombi yetu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.